Friday, January 4, 2019

Wafahamu wachezaji walioko sokoni Ulaya, Ramsey, Morata, Ozil, Higuain, Fabregas na wengine

Kiungo wa kati wa Arsenal Aaron Ramsey, 28, ametia saini makubaliano ya awali ya mkataba na Juventus na huenda akajiunga na klabu hiyo ya Italia mwezi huu. (Sport Mediaset kupitia Calciomercato)



Ramsey ndiye mchezaji wa sasa aliyekaa muda mrefu zaidi Arsenal, alijiunga nao 2008
Mkurugenzi wa michezo wa klabu ya Sevilla Joaquin Caparros anasema klabu hiyo huenda ikawasilisha ofa kumtaka mshambuliaji wa Chelsea ambaye zamani alichezea Real Madrid na Juventus Alvaro Morata, 26. (Football.London)

Kwa mujibu wa BBC, Morata angependa kurejea Madrid iwapo ataondoka Stamford Bridge lakini anaweza tu kuruhusiwa kuondoka iwapo Chelsea watampata mshambuliaji mwingine wakati wa dirisha la kuhama wachezaji la Januari. (Sun)

Hatima ya Mesut Ozil Arsenal haitaamuliwa hadi mwisho wa msimu baada ya kiungo huyo wa miaka 30 na klabu hiyo kupuuzilia mbali uwezekano wake kuhama mwezi huu. (Evening Standard)


Chelsea watafanya uamuzi kumhusu mshambuliaji Tammy Abraham kufikia 14 Januari. Mchezaji huyo wa miaka 21 yupo Aston Villa kwa mkopo lakini anaweza kuitwa kurejea klabu yake wiki mbili baada ya dirisha la kuhama wachezaji kufunguliwa kutokana na maelezo kwenye mkataba wake. (Telegraph)


Chelsea wameamua kutomfuata mshambuliaji wa Argentina Gonzalo Higuain, 31, mwezi huu. Mchezaji huyo kwa sasa yupo AC Milan kwa mkopo kutoka Juventus. (Goal)

Cesc Fabregas hatakubaliwa kukamilisha uhamisho wake kwenda Monaco hadi Chelsea wapate kiungo wa kati wa kujaza nafasi ya Mhispania huyo wa miaka 31. (Calciomercato)


Mlinda lango wa Real Madrid Keylor Navas, 32, ambaye amekuwa akihusishwa na kuhamia Arsenal wiki za hivi karibuni, ameongeza muda wa mkataba wake katika klabu hiyo kwa mwaka mwingine mmoja, hadi Juni 2021. (Marca)


Bayern Munich wamewasilisha ofa ya tatu ya zaidi ya £30m wakimtaka kiungo mshambuliaji wa Chelsea Callum Hudson-Odoi, 18. (Sky Sports)

Beki wa Chelsea mzaliwa wa England Gary Cahill, 33, anakaribia kuhamia Fulham kwa mkopo. Klabu hiyo ya London magharibi imemrejesha Timothy Fosu-Mensah kwa Manchester United ili kutoa nafasi ya mchezaji mwingine ndipo waweze kumchukua Cahill. (Love Sport Radio)

Crystal Palace wamewasilisha ofa ya £6.5m kumtaka mchezaji wa Everton na Senegal Oumar Niasse, 28, baada yao kushindwa kumpata mshambuliaji wa Liverpool Dominic Solanke kwa mkopo. (Sun)

Paris St-Germain wamewasilisha ofa ambayo haiwezi kufikiwa na Barcelona kumtaka kiungo wa kati Frenkie de Jong, 21, na beki wa kati Matthijs de Ligt, 19, kutoka Ajax. (Marca)

Leicester wamepokea ofa kutoka kwa Villarreal ya Uhispania wanaomtaka Vicente Iborra, lakini klabu hizo bado hazijakamilisha mazungumzo kuhusu uhamisho wa Mhispania huyo mwenye miaka 30. (Leicester Mercury)

Chelsea wanapanga kutoa £36m kumtaka winga wa PSV Hirving Lozano, 23, anayetokea Mexico. (Calciomercato, kupitia Talksport)

Cardiff na Bournemouth wote wanamtaka beki wa Liverpool Nathaniel Clyne. Bournemouth wanamtaka mkabaji huyo wa miaka 27 kwa mkopo kwa kipindi kilichosalia cha msimu. (Mail)

Kiungo wa kati wa Liverpool Adam Lallana, 30, anatafutwa na klabu ya Fenerbahce ya Uturuki mwezi huu. (Caught Offside)

Meneja wa Tottenham Mauricio Pochettino amekataa kufutilia mbali uwezekano wa kiungo wa kati wa Ubeligji Mousa Dembele, 31, kuihama klabu hiyo mwezi huu. (Football.London)

Pamoja na Dembele, Tottenham wanataka kuwauza pia Fernando Llorente, 33, Vincent Janssen, 24, Georges-Kevin Nkoudou, 23, na Victor Wanyama, 27. (Mirror


Nottingham Forest wamehusishwa na kumnunua winga wa Portsmouth Jamal Lowe, 24. (Nottingham Post)

Meneja wa zamani wa Birmingham na Derby Gary Rowett huenda akalazimika kuzuia kushindwa mechi ya Kombe la FA ugenini Shrewsbury Jumamosi ili kunusuru kazi yake kama meneja wa Stoke. (Telegraph)

Christian Eriksen anagoma kutia saini mkataba mpya Tottenham, huku mkataba wa sasa wa kiungo huyo wa kati wa Denmark mwenye miaka 26 ukitarajiwa kufikia kikomo baada ya miezi 18. (Evening Standard)


Juventus wamethibitisha kwamba wameonyesha nia ya kumtaka kiungo wa kati wa Arsenal Aaron Ramsey, 28, bila kulipa ada yoyote baada ya mkataba wake kumalizika mwisho wa msimu. (Sky Sports)

Wolves wamewasilisha ofa ya £18m kumtaka mshambuliaji wa Chelsea Tammy Abraham, 21, ambaye kwa sasa yupo kwa mkopo katika klabu ya Aston Villa inayocheza ligi ya Championship. (Sun)

Bournemouth watamruhusu mshambuliaji wa England Jermain Defoe kuondoka klabu hiyo Januari. Mchezaji huyo wa miaka 36 amechezeshwa mara nne pekee kama nguvu mpya ligini msimu huu. (Sky Sports)

Chelsea wanapanga kuendelea kuimarisha kikosi chao mwezi huu hata baada ya kumnunua Christian Pulisic. The Blues bado wanamtaka mshambuliaji wa Bournemouth Callum Wilson, 26, na pia wanamtafuta beki mpya. (Mirror)

Liverpool wanapanga kumpa mshambuliaji wa wao Daniel Sturridge, 29, mkataba mpya. (Mail)

Vituko vya Housegeli na Mama Mwenye Nyumba

Housegirl na mama mwenye nyumba
“Kichekesho cha msichana wa kazi za nyumbani na mama mwenye nyumba juu ya vijiti vya kusafishia meno.
jamani nyie watoto wa nyumba hii, vijiti vya meno nimeleta juzi tu leo vyote vimeisha, mnazipeleka wapi?”
Ndipo housegirl akadakia na kusema “Mama mimi simo humo maana kila nikimaliza kutumia tu navirudishiaga humo humo”

Wednesday, January 2, 2019

MENEJA WA HARMONIZE (MR PUAZ) ASEPA WCB



MENEJA wa mkali wa Bongo Fleva, Rajabu Abdul Kahali maarufu kama Harmonize, Mr Puaz ameacha rasmi kazi ya umeneja kwa msanii huyo; kisa ni kutokuwa na maelewano naye.

Baada ya kusikika kwa tetesi hizo Risasi Mchanganyiko lilimtafuta ‘mzee baba’ huyo ili aweze kuzungumzia kusepa kwake na mwelekeo wake mpya wa kikazi.

“Ni kweli kwa sasa mimi na Harmonize hatufanyi kazi pamoja kwa sababu ya kupishana kauli; lakini haimaanishi mimi na WCB hatufanyi kazi au hatutafanya kazi.

“WCB ni familia yangu ambayo ukaribu wangu na wao ulitokana na urafiki wangu na Diamond hivyo siwezi kuiacha, panapo kuwa na nafasi ya mimi kuhitajika kutoa mchango wangu nitaendelea kutoa kama mwanafamilia,” alisema meneja huyo ambapo Harmonize alipotafutwa jitihada ziligonga mwamba kwa sababu simu yake iliita bila kupokelewa.

MHE. TEMBA KUIREJESHA TMK WANAUME


BAADA ya kila msanii kuoneakana kufanya kazi kivyake, staa wa Bongo Fleva, Amani Temba ‘Mheshimiwa Temba’ amesema Kundi la TMK Wanaume litarudi na kuanza kazi ya muziki kama lilivyokuwa zamani.
Kuthibitisha hilo, Temba alisema anatarajia kuandaa kolabo moja matata mwaka huu wa 2019 ili kurudisha rasmi kundi hilo.
“Nitawalea wimbo ambao utakuwa na vichwa vyote vya TMK Wanaume niliousimamia mimi, nataka kukata kiu ya mashabiki waliokuwa wanatamani kutuona pamoja,” alisema Temba.
Alisema wanatarajia ujio wao huo kuwa wa tofauti kwa kubadilisha mfumo wa utendaji wa kazi kutoka wimbo kuwa na dakika tano na kuwa dakika tatu.
Kundi la TMK Wanaume lilikuwa likiundwa na mastaa kibao wakiwemo Temba, Juma Nature, Y Dash, Chegge, Inspector Haroun, Dolo, Rich One na KR.
Kundi hilo lilianza kugawanyika kwa baadhi ya mastaa wakiongozwa na Nature, Dolo, Rich One na KR kujitoa kundini na kuanzisha kundi lao la Wanaume Halisi.

AJIBU AMPA MAKAMBO MABAO MANNE BARA

Mshambuliaji Heritier Makambo
KIUNGO mshambuliaji wa Yanga, Ibrahim Ajibu, amekuwa msaada mkubwa kwa mshambuliaji Heritier Makambo ambaye kwa sasa anaongoza kwa ufungaji akiwa na mabao 11 kwenye Ligi Kuu Bara msimu huu.

Ajibu ambaye mpaka sasa ana asisti 13 msimu huu, amehusika katika mabao manne kati ya 11 yaliyofungwa na Makambo.

Katika jumla ya mabao 35 ambayo Yanga imeyafunga mpaka sasa kwenye ligi hiyo ikiwa na pointi 50 kileleni, Ajibu ameonekana kumtengenezea Makambo nafasi nyingi za kufunga kuliko mchezaji yeyote kikosini hapo.

Asisti ambazo Ajibu amempatia Makambo mpaka sasa ni katika mchezo dhidi ya Coastal Union ambao ulichezwa kwenye Uwanja wa Taifa ambapo Yanga iliibuka na ushindi wa bao 1-0.

Pia katika mchezo dhidi ya Alliance ambao nao ulichezwa Uwanja wa Taifa, Yanga walishinda mabao 3-0, Ajibu alimpa asisti moja Makambo. Mechi dhidi ya Ruvu Shooting iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Yanga walishinda 3-2 na Ajibu alimpa Makambo asisti moja, huku asisti ya nne ya Ajibu kwa Makambo ilikuwa kwenye mchezo dhidi ya Mbeya City ambapo Yanga ilishinda 2-1 kwenye Uwanja wa Sokoine, Mbeya.

MBELGIJI WA SIMBA AIGOMEA YANGA SC

Mbelgiji, Patrick Aussems.
KOCHA mkuu wa Simba, Mbelgiji, Patrick Aussems amesema katika mechi zao 24 za Ligi Kuu Bara zilizobaki, hawatafungwa kwenye uwanja wao wa nyumbani kwa lengo la kuipiku Yanga na kutetea ubingwa wao.

Mbelgiji huyo alisema kuwa licha ya wapinzani wao Yanga kuwa juu katika msimamo wa ligi hiyo siyo kigezo cha wao kushindwa kutetea ubingwa wao.

Yanga inaongoza msimamo wa ligi kuu kwa pointi 50 baada ya mechi 18 huku Simba ikiwa na alama 33 katika michezo 14 ikiwa na viporo vinne.
Kikosi cha timu ya Simba.
Katika mechi 24 ambazo Simba imesalia kuzicheza msimu huu imesaliwa na mechi takribani 13 dhidi ya Azam (2), Yanga, Mbao, Mtibwa Sugar, Coastal Union, KMC, Kagera Sugar, JKT Tanzania, Ndanda, Mwadui FC, Ruvu Shooting, Biashara United mechi hizo zote zitachezwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Championi Jumatano, kocha huyo alisema kuwa mahesabu ya kushinda mechi za nyumbani ni muhimu ili kutetea ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu wa mwaka 2018/19.

“Sina hofu na spidi ya Yanga katika ligi na Azam hawanitishi sababu mpango wangu baada ya mechi ya Singida ni kushinda mechi zote ambazo tutakuwa katika uwanja wa nyumbani mpaka msimu unamalizika katika mechi 24 zilizosalia.
“Timu yangu itakaposhinda mechi zote za nyumbani ni wazi nafasi ya kutetea ubingwa kwetu iko palepale na ni lazima kupambana kwa hilo sababu ndiyo nafasi pekee ambayo tumesalia nayo ili msimu ujao tushiriki tena michuano ya kimataifa kama ilivyo sasa,” alisema Mbelgiji huyo.

Huyu ndio mchezaji mpira tajiri kuliko wote duniani

Sio Christiano Ronaldo
Sio King Leonel Messi

Ni Faiq Bolkiah. Anachezea club ya leicester city reselve team. Katika umri wa miaka 20 anamiliki utajiri wa US$ 20 billion.
Ni nephew wa sultan wa Brunei. 
screenshot_20180111-185623-png.673147

1515685876045-jpg.673148